• Contact Us |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
    • Complaints |
Dar es Salaam City Council
Dar es Salaam City Council

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government Dar es Salaam City Council

  • Home
  • About Us
    • City Profile
    • Mission and Vision
    • Core Values
    • Council Strategies
  • Administration
    • Organization Structure
    • Department
      • Finance, Administration and Personnel
      • Works and Fire Rescue
      • Waste Management
      • Urban Planning, Environment and Transportation
      • Health Services
    • Units
      • Planning, Monitoring and Statistics
      • Legal and Safety
      • Public Relations and Protocol
      • Internal Audit
      • Procurement and Supply
  • Investment Opportunity
    • Tourism Activities
      • Our Dar es Salaam
      • Animal zoos
      • Cultural Arts and Traditions
      • Dar es Salaam Centre for Architectural Heritage
      • Public spaces, Garden and Sports
      • Shopping, Entertainment and Social life
      • Historical and Heritage building and sites
      • Beaches, Waterfronts and Islands
    • Recycling of Solid Waste
  • Our Services
    • Motorcycle Permit
    • Taxi Parking Permit
    • Car Parking
    • Bus Terminals
    • Solid Waste Management
    • Land History Information
    • Burial for unclaimed dead bodies
  • Councillors
    • All Councillors
    • Standing Committee
      • Finance and Administration Committee
      • Urban Planning, Environment and Infrastructure Commitee
      • Planning and Coordination Committee
      • Social Welfare Committee
      • Ethics Committee
    • Council Meetings
    • Lord Mayor's Timetable
    • Former City Mayors
  • Projects
    • Completed projects
    • Planned Projects
    • Ongoing Projects
    • City Investments
  • Publications
    • Acts
    • ByLaws
    • Policies
    • Guidelines
    • Reports
    • Application Form
    • Integrity Pledges Form
  • Media Centre
    • Press Release
    • Photo Gallery
    • Video Gallery
    • Speeches
    • News
    • Events

RC Makalla Aongoza Maadhimisho ya Siku ya Wanawake Duniani Mkoa wa Dar es Salaam

Posted on: March 8th, 2023

Kila Tarehe 08 Machi Taifa linaadhimisha siku ya Wanawake Duniani ambapo Leo Machi 08, 2023 maadhimisho hayo katika Mkoa wa Dar es Salaam yameweza kuadhimishwa katika viwanja Vya Mnazi Mmoja Jijini Dar es Salaam huku mgeni rasmi akiwa ni Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Mhe. Amos Makalla.

Katika maadhimisho hayo yenye kauli mbiu isemayo "UBUNIFU NA MABADILIKO YA TEKNOLOJIA NI CHACHU KATIKA KULETA USAWA WA KIJINSIA" yameweza kubeba sura ya Kongamano la Wanawake na Fursa za Kiuchumi, yaliwapa nafasi kina mama na vikundi mbalimbali vya ujasiriamali kushiriki, kuonyesha bidhaa zao, na kuuza bidhaa hizo.

Akiongea katika maadhimisho hayo Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Mhe.Amos Makalla amesema “Kwanza kabisa napenda kutoa shukrani zangu za dhati kwa Rais wa Jamuhuri ya Muunguno wa Tanzania Mhe.Samia Suluhu Hassan kwa kuweza kuwawezesha Wanawake kiuchumi kupitia mikopo ya Halmashauri kwani Billioni 13.9 zimeweza kutolewa kwaaajili ya kusaidia vikundi vya Wanawake,Vijana pamoja na watu wenye ulemavu ikiwa bilioni 6.1 wamepewa Wanawake huku bilioni 5.9 zikielekezwa katika vikundi vya Vijana na bilioni 1.8 zikielekezwa katika vikundi vya watu wenye ulemavu ambapo takribani vikundi 1243 vimeweza kunufaika na mikopo hiyo ikiwa vikundi 69 ni vya wanawake vukundi 428 ni za vijana na vikundi 126 vikiwa ni vya watu wenye ulemavu hivyo natoa wito kwa wananchi wa mkoa wa Dar es Salaam mjitokeze kwa wingi kunufaika na fursa hii ya mkopo wa asilimia 10%ya mapato ya ndani ya Halmashauri ili muweze kujikwamua kiuchumi pia kwa wale ambao mshapata mikopo hiyo mhakikishe mnarejesha fedha hizo kwa wakati ili wengine nao waweze kupata mkopo.”

Aidha Mhe Makalla ameendelea kusema “Mimi kama kiongozi wa Serikali nimeona niwaoneshe kwamba ninaheshimu Wanawake na kuthamini juhudi zao wanazozifanya kuhusu usawa wa kijinsia na uwezeshaji wa wanawake kiuchumi ambapo leo hii duniani kote wanaadhimisha siku ya Wanawake kama sisi Tanzania ambapo kitaifa hufanyika kila baada ya Miaka mitano, na Kila Mwaka kila Mkoa hufanya katika Mkoa wake lengo likiwa kuwawezesha Wanawake kujikwamua Kiuchumi, kielimu,kiafya pamoja na kuwawezesha wajasiriamali.”

Sambamba na hilo Mhe. Makalla ameweza kuzishukuru Taasisi, Mashirika na Makampuni binafsi ambayo yameweza kuwaruhusu wanawake kuweza kuungana na wanawake wengine siku hii ya leo niwaase Wanawake kuwa wamoja katika kutetea haki zenu na Taifa letu kwa ujumla na ndio maana hata mimi nimeheshimu siku hii nakuweza kuungana na ninyi.

Vilevile Mhe.Makalla aliweza kukagua mabanda ya wajasiriamali kutoka Halmashauri zote zaMkoa wa Dar es Salaam ambao ni wanufaika wa Mkopo wa asilimia 10% za mapato ya ndani ya Halmashauri ambapo aliweza kujionea bidhaa mbalimbali wanazotengeneza wanawake wajasiriamali huku akitoa rai kwa wanawake kuhakikisha wanapata mafunzo ili waweze kupata Masoko ya ndani na nje, “Kadri uchumi unavyokua fursa zinazidi kuongezeka hivyo naamini kwa mikono ya Wanawake, Masoko tunayo hivyo nitoe wito kwa wanawake wathibiti ubora wote kuwatia wanawake wengine moyo tusiwakatishe tamaa ili waweze kukua kiuchumi pia nitoe wito kwa Jamii kujenga tabia ya kununua bidhaa zinazozalishwa kwa mikono ya wajasiriamali wenzetu na pia wajasiriamali mhakikishe mnatengeneza bidhaa zinazokidhi ubora na viwango ili muweze kupata Masoko ndani na nje ya nchi.” Amesisitiza Mhe. Makalla.

Kwa upande wake Mkuu wa Wilaya ya Ilala Mhe. Edward Mpogolo ambaye ni mwenyeji katika maadhimisho haya yaliyofanyika katika Wilaya ya Ilala amesema “Kwa niaba ya Wakuu wenzangu wa Wilaya Nyingine nipende kuwapongeza wamama wa Halmashauri zote za Mkoa wa Dar es Salaam ambao wameweza kujiajiri kupitia mkopo wa Asilimia 10% za mapato ya ndani ambapo hii leo wameweza kutambulisha bidhaa zao hivyo nipende kukushukuru Mkuu wa Mkoa Wa Dar es Salaam kwa kuungana na Wanawake hawa katika Siku yao hii Muhimu pia nikuhakikishie wakani Mimi na Wakuu wa Wilaya wenzangu tutafanya jambo kwa ajili ya kuwawezesha Wanawake hawa wajasiriamali wa Mkoa wa Dar es Salaam kujikwamua Kiuchumi.”

Akiongea kwa niaba ya Vikundi vya Wajasiriamali kutoka Mkoa wa Dar es Salaam vinavyonufaika na mikopo ya asilimia 10 %ya Halmshauri mjasiriamali wa Kikundi cha wethy kutoka Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam Bibi.Letisia Pius Rutta amesema “Tunaishukuru Serikali ya Tanzania inayoongozwa na Rais Samia Suluhu Hassan katika kutekeleza Ilani ya Chama cha Mapindunzi na Sera mbalimbali hasa kumuinua Mwanamke Kiuchumi ameweza kutupatia mikopo na kuanzisha majukwaa mbalimbali yanayotetea haki za Wanawake hivyo tunamuahidi tutatumia fursa hii kujikwamua Kiuchumi.”

Announcements

  • TAARIFA KWA UMMA February 19, 2025
  • TAARIFA KWA UMMA - MATUMIZI YA NISHATI SAFI YA KUPIKIA January 17, 2025
  • MATOKEO YA UPIMAJI WA KITAIFA WA DARASA LA NNE (SFNA) 2024 January 04, 2025
  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA KWANZA, 2025 December 16, 2024
  • View All

Latest News

  • "Tutahakikisha tunasimamia Kata 36 na Mitaa 159 ili Jiji la DSM liwe safi" - DC Mpogolo

    May 03, 2025
  • Jiji La DSM laweka mikakati kushinda UMITASHUMTA ngazi ya Mkoa

    April 29, 2025
  • Wakazi wa Jiji la Dar es Salaam waadhimisha Muungano kwa kupanda miti na kufanya usafi wa mazingira

    April 26, 2025
  • Zoezi la usafi wa mwisho wa wiki laendelea

    April 12, 2025
  • View All

Video

Msimbazi Basin Development Project Implementation Area
More Videos

Quick Links

  • Former City Council Mayors
  • Motorcycle's Permit
  • Solid Waste Management
  • Smart Area
  • Dar es Salaam Centre for Architectural Heritage
  • Beaches, Waterfronts and Islands
  • Cultural Arts and Traditions
  • Historical and Heritage building and sites
  • Public spaces, Garden and Sports

Related Links

  • BUNGE
  • Blogu ya Jiji
  • UTUMISHI
  • State House
  • Ilala Municipal Council
  • Tanzania Information Services

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Location Map

Contact Us

    1 BARABARA YA MOROGORO 11882 DAR ES SALAAM

    Postal Address: S.L.P 20950

    Telephone: 0738 378 386

    Mobile: 0738 378 386

    Email: info@dcc.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclaimer
    • Sitemap

Copyright © 2017 Dar es Salaam City Council . All rights reserved.