• Contact Us |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
    • Complaints |
Dar es Salaam City Council
Dar es Salaam City Council

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government Dar es Salaam City Council

  • Home
  • About Us
    • City Profile
    • Mission and Vision
    • Core Values
    • Council Strategies
  • Administration
    • Organization Structure
    • Department
      • Finance, Administration and Personnel
      • Works and Fire Rescue
      • Waste Management
      • Urban Planning, Environment and Transportation
      • Health Services
    • Units
      • Planning, Monitoring and Statistics
      • Legal and Safety
      • Public Relations and Protocol
      • Internal Audit
      • Procurement and Supply
  • Investment Opportunity
    • Tourism Activities
      • Our Dar es Salaam
      • Animal zoos
      • Cultural Arts and Traditions
      • Dar es Salaam Centre for Architectural Heritage
      • Public spaces, Garden and Sports
      • Shopping, Entertainment and Social life
      • Historical and Heritage building and sites
      • Beaches, Waterfronts and Islands
    • Recycling of Solid Waste
  • Our Services
    • Motorcycle Permit
    • Taxi Parking Permit
    • Car Parking
    • Bus Terminals
    • Solid Waste Management
    • Land History Information
    • Burial for unclaimed dead bodies
  • Councillors
    • All Councillors
    • Standing Committee
      • Finance and Administration Committee
      • Urban Planning, Environment and Infrastructure Commitee
      • Planning and Coordination Committee
      • Social Welfare Committee
      • Ethics Committee
    • Council Meetings
    • Lord Mayor's Timetable
    • Former City Mayors
  • Projects
    • Completed projects
    • Planned Projects
    • Ongoing Projects
    • City Investments
  • Publications
    • Acts
    • ByLaws
    • Policies
    • Guidelines
    • Reports
    • Application Form
    • Integrity Pledges Form
  • Media Centre
    • Press Release
    • Photo Gallery
    • Video Gallery
    • Speeches
    • News
    • Events

Wakuu wa Shule za Sekondari Jiji la DSM waaswa kuongoza kwa kufuata sheria, kanuni na taratibu

Posted on: August 31st, 2021

Na; Judith Msuya.

Wakuu wa Shule za Sekondari za Umma pamoja na za Binafsi za Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam leo Augusti 21, 2021 wamefanya kikao kazi kwa ajili ya maandalilizi ya kuwapokea wanafunzi wa kidato cha kwanza mwaka 2022, kikao hicho  kilichofanyika katika ukumbi wa Shule ya Sekondari ya Shaabani Robert Jijini Dar es Salaam kimehudhuriwa pia na Mkuu wa Wilaya ya Ilala, Meya wa Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam, Maafisa Elimu kata pamoja na mafundi ujenzi wanaotumika kujenga Shule mbalimbali.

Akizungumza katika kikao kazi hicho Mkuu wa Wilaya ya Ilala Mhe. Ng'wilabuzu Ludigija amesema kuwa wanafunzi takribani 28,480 wanatarajiwa kufanya mtihani wa darasa la saba mwaka huu ambapo makadirio ya wanafunzi watakao faulu wanatarajiwa kuwa Wanafunzi 26,800 ambao ni idadi kubwa na wanatakiwa kuingia darasani kwa wakati hivyo maandalizi lazima yafanyike mapema ili ifikapo Januari 2022 Wanafunzi wote watakaofaulu waweze kuingia darasani kwa wakati.

"Tumetenga fedha takribani milioni 900 kwaajili ya kuongeza madarasa na kununua vifaa vya shule Kwa baadhi ya Shule kwa ajili ya Wanafunzi watakao faulu kuingia kidato cha kwanza 2022 hivyo fedha hizo zitatolewa mapema ili taratibu za utekelezaji zianze kusudi tuweze kuepusha usumbufu uliojitokeza mwaka 2021 ambapo Wanafunzi walichelewa kuanza masomo kwa wakati muafaka kutokana na ujenzi kuchelewa kukamilika". alisema Mhe. Ludigija.

Sambamba na hilo Mkuu wa Wilaya amewasisitiza Wakuu wa Shule hao kuhakikisha wanatunza  nyaraka zote za malipo ya Miradi, barua za vikao pamoja na nyaraka zote za muhtasari wa vikao vyao zinahifadhiwa vizuri kwa ajili ya kumbukumbu za badaye bila kusahau kuwashirikisha wananchi wanaowazunguka kwani pamoja na kwamba fedha zinatolewa na Serikali lakini miradi hiyo inawahusu Wananchi hivyo sibudi kuwashirikisha Wananchi hao ili kufanya mambo kuwa mepesi katika utekelezaji wa miradi ya maendeleo ya ujenzi wa shule.

Kwa upande mwingine Mhe. Ludigija aliwapongeza Wakuu wa Shule kwa ushirikiano mzuri baina yao na viongozi wao kutoka ofisi ya Mkurugenzi wa Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam kwa kazi kubwa waliyoifanya kwa kipindi cha mwaka wa fedha 2021 kwa kujenga madarasa takribani 178 kwa muda mfupi  na hivyo kuwaagiza Wakuu wa shule kuhakikisha kuwa kuelekea kipindi hiki cha mitihani wahakikishe wanafunzi wote wamesajiliwa kama inavyotakiwa ili kuepusha usumbufu unaojitokeza kwa wanafunzi na Wazazi katika kipindi cha mitihani.

"Nawashukuru sana kwa mchango wenu na nawaahidi kushirikiana na nyinyi katika utekelezaji wa miundombinu, kudumisha michezo, nidhamu pamoja na taaluma katika shule zetu ili kuhakikisha Halmashauri yetu ya Jiji la Dar es Salaam inakua kinara katika kuboresha Elimu na Pia niwaombe 'local Fundi' unapopata kazi kwenye Jiji la Dar es Salaam unaikamilisha kwa wakati ili kuepusha usumbufu kwa Walimu wakuu wa Shule ambao wanasimamia Taaluma kwa watoto wetu."

Kikao kazi hicho kilicho funguliwa na Afisa Elimu Mkoa wa Dar es Salaam Ndug.Abdul Maulid ambaye amewasisitiza Wakuu wa Shule za Sekondari za Halmashauri ya Jiji la Dar es salaam  kuhakikisha wanasimamia shule katika misingi ya kisheria, taratibu na kanuni katika kusimamia nidhamu ya Shule, usafi wa mazingira, ulinzi na usalama, michezo na burudani  pamoja na kuhakikisha wanasimamia vyema miundombinu ya Shule ili kuhakikisha fedha zinazotolewa na Serikali kwenye 'Force Account' kwa lengo la kuboresha miundombinu ya shule zinatumika vyema ili kuhakikisha ujenzi bora wa majengo ya shule unakamilika kwa wakati na unatekelezwa kwa kiwango cha hali ya juu.

Aidha, kikao hicho kilifikia tamati kwa Wakuu wa Shule kuweza kutoa maoni yao na kuahidi kuwa watatekeleza yote waliyoagizwa kuyafanya ikiwemo suala zima la usimamizi wa miundombinu ya Shule na Taalumu kwa ujumla.

Announcements

  • TAARIFA KWA UMMA February 19, 2025
  • TAARIFA KWA UMMA - MATUMIZI YA NISHATI SAFI YA KUPIKIA January 17, 2025
  • MATOKEO YA UPIMAJI WA KITAIFA WA DARASA LA NNE (SFNA) 2024 January 04, 2025
  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA KWANZA, 2025 December 16, 2024
  • View All

Latest News

  • "Tutashirikiana na CRDB kuhakikisha mradi unakamilika kwa wakati" - DC Mpogolo

    June 22, 2025
  • Naibu Spika atembelea eneo la ujenzi wa shule ya mfano ya CRDB

    June 22, 2025
  • Kata kwa Kata, Mtaa kwa Mtaa kutoa elimu ya mikopo ya asilimia 10 - DC Mpogolo

    June 20, 2025
  • "Mikopo ya asilimia 10 ni silaha ya kuinua uchumi wa wananchi" - DC Mpogolo

    June 20, 2025
  • View All

Video

Msimbazi Basin Development Project Implementation Area
More Videos

Quick Links

  • Former City Council Mayors
  • Motorcycle's Permit
  • Solid Waste Management
  • Smart Area
  • Dar es Salaam Centre for Architectural Heritage
  • Beaches, Waterfronts and Islands
  • Cultural Arts and Traditions
  • Historical and Heritage building and sites
  • Public spaces, Garden and Sports

Related Links

  • BUNGE
  • Blogu ya Jiji
  • UTUMISHI
  • State House
  • Ilala Municipal Council
  • Tanzania Information Services

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Location Map

Contact Us

    1 BARABARA YA MOROGORO 11882 DAR ES SALAAM

    Postal Address: S.L.P 20950

    Telephone: 0738 378 386

    Mobile: 0738 378 386

    Email: info@dcc.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclaimer
    • Sitemap

Copyright © 2017 Dar es Salaam City Council . All rights reserved.