• Contact Us |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
    • Complaints |
Dar es Salaam City Council
Dar es Salaam City Council

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government Dar es Salaam City Council

  • Home
  • About Us
    • City Profile
    • Mission and Vision
    • Core Values
    • Council Strategies
  • Administration
    • Organization Structure
    • Department
      • Finance, Administration and Personnel
      • Works and Fire Rescue
      • Waste Management
      • Urban Planning, Environment and Transportation
      • Health Services
    • Units
      • Planning, Monitoring and Statistics
      • Legal and Safety
      • Public Relations and Protocol
      • Internal Audit
      • Procurement and Supply
  • Investment Opportunity
    • Tourism Activities
      • Our Dar es Salaam
      • Animal zoos
      • Cultural Arts and Traditions
      • Dar es Salaam Centre for Architectural Heritage
      • Public spaces, Garden and Sports
      • Shopping, Entertainment and Social life
      • Historical and Heritage building and sites
      • Beaches, Waterfronts and Islands
    • Recycling of Solid Waste
  • Our Services
    • Motorcycle Permit
    • Taxi Parking Permit
    • Car Parking
    • Bus Terminals
    • Solid Waste Management
    • Land History Information
    • Burial for unclaimed dead bodies
  • Councillors
    • All Councillors
    • Standing Committee
      • Finance and Administration Committee
      • Urban Planning, Environment and Infrastructure Commitee
      • Planning and Coordination Committee
      • Social Welfare Committee
      • Ethics Committee
    • Council Meetings
    • Lord Mayor's Timetable
    • Former City Mayors
  • Projects
    • Completed projects
    • Planned Projects
    • Ongoing Projects
    • City Investments
  • Publications
    • Acts
    • ByLaws
    • Policies
    • Guidelines
    • Reports
    • Application Form
    • Integrity Pledges Form
  • Media Centre
    • Press Release
    • Photo Gallery
    • Video Gallery
    • Speeches
    • News
    • Events

Waziri Gwajima awataka Wajasiriamali kujiunga na majukwaa ya wanawake ili kutangaza biashara zao

Posted on: September 11th, 2023

Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum, Mhe. Dkt. Dorothy Gwajima amewataka wajasiriamali kujiunga na majukwaa ya wanawake lengo likiwa ni kurasimisha biashara zao ili waweze kufanya biashara kwa wigo mpana zaidi.

Mhe. Dkt. Gwajima ameyasema hayo tarehe 11 Septemba, 2023 katika ufunguzi wa Maonesho ya Wajasiriamali yaliyoandaliwa na Taasisi ya CRDB Bank kwa kushirikiana na Ofisi ya Mkuu wa Wilaya Ya Ilala yenye kauli mbiu isemayo ‘Asante Rais Samia biashara zimefunguka’ lengo likiwa ni kutoa muamko kwa wajasiriamali ili waweze kuchangamkia fursa mbalimbali zinazopatikana baada ya kujiunga na majukwaa mbalimbali yanayoambatana na elimu ya ujasiriamali.

Aidha Dkt. Gwajima ameongeza kuwa ili kwenda na wakati na kupata fursa zinazotokea katika mchakato mzima wa ununuzi ni vyema wajasiriamali wakarasimisha biashara zao na kujiunga na majukwaa ya wanawake kwani Sekta binafsi zinaonesha mchango mkubwa wa kuwakwamua wanawake na vijana ili kukuza uchumi wa taifa letu.

“Nipende kumshukuru Raisi wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzanzia Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuamua kuunda Wizara hii ili ishirikiane na ninyi kwani kuna faida nyingi kwenye majukwaa hivyo wanawake mnyanyuane mfike kwenye majukwaa fursa zipo muachane na mikopo yenye riba kubwa nendeni ‘Imbeju’ kuna fursa.” Ameeleza Dkt. Gwajima.

Vilevile Dkt. Gwajima ametoa shukrani zake kwa CRDB Bank na Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Ilala kwa kuanzisha maonesho haya endelevu huku akiahidi kuitangaza programu yao ya ‘imbeju’ wakati anapokua kwenye mikutano yake mbalimbali lengo likiwa ni kuhakikisha wajasiriamali wote wanapata elimu za kuboresha bidhaa zao na kupata masoko zaidi.

Akiongea kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Mkuu wa Wilaya ya Ilala Mhe. Edward Mpogolo ameeleza kuwa “Katika kuwawezesha wananchi kiuchumi, Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Ilala kupitia Idara ya Maendeleo ya Jamii tulishirikiana na CRDB Bank ambapo walitueleza juu ya Programu ya Imbeju huku na sisi tukiwa na Asilimia 10 ya mapato ya ndani ya Halmashauri hivyo tuliona ni vyema kuungana kuanziasha maonesho haya lengo likiwa ni kutengeneza masoko kwa wajasiriamali wetu na kuwapa elimu juu ya ujasiriamali. Hivyo tunawashukuru sana CRDB Bank foundation kwa kuanzisha programu ya Imbeju ambayo imekua chachu ya wajasiriamali kujipatia mikopo mbalimbali kwaajili ya kuendeleza biashara zao na kujikwamua kiuchumi.”

Naye Mkurugenzi Mtendaji wa CRDB Bank Ndg. Abdulmajid Mussa Nsekela ameleza kuwa katika kuwakwamua wanawake na vijana Wajasiriamali elfu 65 wamefikiwa na programu ya imbeju huku mikopo ya zaidi ya shilingi Milion 200 zikitolewa kwa baadhi ya vikundi vya wajasiriamali.

Aidha katika maonesho hayo mikopo mbalimbali ilikabidhiwa kwa baadhi ya wajasiriamali ikiwepo mikopo ya bajaji, pikipiki pamoja na fedha taslimu.

Maonesho haya ni bure na yatafanyika kwa siku tatu kuanzia leo tarehe 11 hadi 13 ambapo wananchi watapewa elimu mbalimbali juu ya ujasiriamali na jinsi ya kutafuta masoko ndani ya nchi na nje ya nchi.

Announcements

  • TAARIFA KWA UMMA February 19, 2025
  • TAARIFA KWA UMMA - MATUMIZI YA NISHATI SAFI YA KUPIKIA January 17, 2025
  • MATOKEO YA UPIMAJI WA KITAIFA WA DARASA LA NNE (SFNA) 2024 January 04, 2025
  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA KWANZA, 2025 December 16, 2024
  • View All

Latest News

  • Mwenge wa Uhuru waweka jiwe la Msingi Kituo cha Afya Mzinga

    June 03, 2025
  • Mwenge wa Uhuru wakagua mradi wa vijana "Ulipo Tupo" Tabata

    June 03, 2025
  • Mradi wa Ujenzi wa Barabara ya Magengeni - Chang'ombe umewekewa jiwe la msingi na Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru Kitaifa

    June 03, 2025
  • Mwenge wa Uhuru wazindua mradi wa Nishati Safi Soko la Samaki Feri

    June 03, 2025
  • View All

Video

Msimbazi Basin Development Project Implementation Area
More Videos

Quick Links

  • Former City Council Mayors
  • Motorcycle's Permit
  • Solid Waste Management
  • Smart Area
  • Dar es Salaam Centre for Architectural Heritage
  • Beaches, Waterfronts and Islands
  • Cultural Arts and Traditions
  • Historical and Heritage building and sites
  • Public spaces, Garden and Sports

Related Links

  • BUNGE
  • Blogu ya Jiji
  • UTUMISHI
  • State House
  • Ilala Municipal Council
  • Tanzania Information Services

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Location Map

Contact Us

    1 BARABARA YA MOROGORO 11882 DAR ES SALAAM

    Postal Address: S.L.P 20950

    Telephone: 0738 378 386

    Mobile: 0738 378 386

    Email: info@dcc.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclaimer
    • Sitemap

Copyright © 2017 Dar es Salaam City Council . All rights reserved.