• Contact Us |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
    • Complaints |
Dar es Salaam City Council
Dar es Salaam City Council

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government Dar es Salaam City Council

  • Home
  • About Us
    • City Profile
    • Mission and Vision
    • Core Values
    • Council Strategies
  • Administration
    • Organization Structure
    • Department
      • Finance, Administration and Personnel
      • Works and Fire Rescue
      • Waste Management
      • Urban Planning, Environment and Transportation
      • Health Services
    • Units
      • Planning, Monitoring and Statistics
      • Legal and Safety
      • Public Relations and Protocol
      • Internal Audit
      • Procurement and Supply
  • Investment Opportunity
    • Tourism Activities
      • Our Dar es Salaam
      • Animal zoos
      • Cultural Arts and Traditions
      • Dar es Salaam Centre for Architectural Heritage
      • Public spaces, Garden and Sports
      • Shopping, Entertainment and Social life
      • Historical and Heritage building and sites
      • Beaches, Waterfronts and Islands
    • Recycling of Solid Waste
  • Our Services
    • Motorcycle Permit
    • Taxi Parking Permit
    • Car Parking
    • Bus Terminals
    • Solid Waste Management
    • Land History Information
    • Burial for unclaimed dead bodies
  • Councillors
    • All Councillors
    • Standing Committee
      • Finance and Administration Committee
      • Urban Planning, Environment and Infrastructure Commitee
      • Planning and Coordination Committee
      • Social Welfare Committee
      • Ethics Committee
    • Council Meetings
    • Lord Mayor's Timetable
    • Former City Mayors
  • Projects
    • Completed projects
    • Planned Projects
    • Ongoing Projects
    • City Investments
  • Publications
    • Acts
    • ByLaws
    • Policies
    • Guidelines
    • Reports
    • Application Form
    • Integrity Pledges Form
  • Media Centre
    • Press Release
    • Photo Gallery
    • Video Gallery
    • Speeches
    • News
    • Events

Waziri Mkuu aelekeza Afua zote za Ugonjwa wa Malaria Kusimamiwa Vizuri ili kuweza kutokomeza kabisa Malaria Nchini

Posted on: April 25th, 2023

Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kushirikiana na wadau wa Sekta ya Afya imepiga hatua kubwa kwenye mapambano dhidi ya ugonjwa wa malaria Nchini, hayo yamebainishwa na Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Majaliwa Kassim Majaliwa leo Aprili 23, 2023 kwenye maadhimisho ya Siku ya Malaria Duniani ambayo Kitaifa yamefanyika Jijini Dar es Salaam katika viwanja vya Mnazi Mmoja.

“Tumepiga hatua kubwa kwenye mapambano dhidi ya Ugonjwa wa Malaria, tumeweza kupunguza kiwango cha maambukizi kutoka asilimia 14.8 mwaka 2015 hadi kufikia asilimia 8.1 mwaka 2022." amesema Waziri Mkuu Majaliwa.

Mhe. Majaliwa amesema kauli mbiu ya maadhimisho ya siku ya malaria duniani kwa mwaka huu ambayo ni ‘Wakati wa kutokomeza Malaria ni sasa, Badilika, Wekeza, Tekeleza. Ziro Malaria inaanza na Mimi’ itekelezwa kwa vitendo kwa kuwa inaenda sambamba na utekelezaji wa Ilani ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) Ibara ya 83 (M,N,O) ya utekelezaji wa mkakati wa Serikali kwenye Mapambano dhidi ya Malaria.

“Ilani ya Chama Cha Mapinduzi imetoa maelekezo kwa Serikali, kuendelea kuihamasisha jamii juu ya matumizi ya vyandarua vilivyowekwa dawa, kupulizia viuwatilifu ukoko kwenye nyumba, kutekeleza mpango wa kuangamiza viluilui vya mbu na kutoa hamasa katika mapambano dhidi ya magonjwa ya kuambukiza” ameeleza Waziri Mkuu.

Aidha katika maadhimisho hayo Mhe. Majawiliwa amezindua gari maalumu litakalotumika katika shughuli mbalimbali za utafiti juu ya ugonjwa wa Malaria pamoja na Uzinduzi wa baraza la kupambana na Malaria lenye wajumbe 19 huku akiwasisitiza kuhakikisha wanafanya kampeni za kudhibiti ugonjwa huo kwa kuanza na Mikoa ambayo iko chini ya asilimia moja ili kutokomeza kabisa ugonjwa huo.

Katika kutelekeza kwa Vitendo mapambano dhidi ya ugonjwa wa malaria, Waziri Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa amesema kuwa Mheshimiwa Rais Samia Suluhu Hassan ametoa unafuu kwa watanzania kwa kupata huduma za tiba ya ugonjwa wa malaria bure, ikiwemo Vipimo vya MRDT, Dawa za Aru, Sindano ya Malaria kali, Dawa za SP kwa ajili ya kutibu Malaria kwa wajawazito vyote vitatolewa bure kuanzia sasa.

Kwa upande wake Waziri wa Afya Mhe. Ummy Mwalimu amesema Serikali imeendelea na mapambano dhidi ya kutokomeza ugonjwa huo na hadi kufikia mwaka 2022, idadi ya Mikoa yenye kiwango cha maambukizi ya malaria chini ya asilimia moja imefikia 9 (Arusha, Kilimanjaro, Manyara, Dodoma, Singida, Iringa, Dar es Salaam, Songwe na Mwanza) kutoka Mikoa 6 mwaka 2017 hivyo kufanya asilimia ya watu wanaoishi katika maeneo yenye malaria chini ya asilimia moja kufikia asilimia 41.

Sambamba na hilo Mhe. Ummy amesema Serikali kupitia Wizara ya Afya imeweka kipaumbele kikubwa kwenye mapambano ya kutokomeza ugonjwa wa Malaria ifikapo Mwaka 2030 hivyo ni vyema Wadau wa Sekta ya Afya kwenye mapambano dhidi ya Malaria wakaunganisha nguvu za pamoja na Serikali katika utekelezaji wa afua za mapambano dhidi ya ugonjwa huo na kuweza kuutokomeza nchini.

Akitoa Shukrani zake kwa Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Mhe. Amos Makalla amesema “Tunamshukuru Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kutoa fedha zaidi ya bilioni 37 kwaajili ya kuboresha huduma za Afya katika Mkoa wa Dar es Salaam kwani fedha hizo zimetumika katika kujenga Zahanati, vituo vya Afya pamoja na kuboresha huduma mbalimbali katika Hospitali za Wilaya ambazo zinaendana na kasi za utokomezaji wa ugonjwa wa malaria pia tunashukuru kwani Wananchi wa Mkoa wa Dar es Salaam wameweza kupata elimu ya jinsi ya kujikinga na Malaria ambapo Mkoa wa Dar es Salaam umeweza kupunguza maambukizi ya ugonjwa wa malaria kwa asilimia kubwa kutoka asilimia 6% Mpaka kufikia 0.9% za maambukizi hii inatokana na kampeni ya ‘Safisha Pendezesha Dar es Salaam’ ambayo imeonesha mafanikio makubwa kwani Wananchi wamekua wakisafisha mitaro ya maji, kufyeka majani, kiziba madimbwi ya maji bila kusahau kulala kwenye chandarua hivyo naamini Mkoa wa Dar es Salaam utakua wa kwanza kutokomeza ugonjwa wa Malaria Nchini”.

Announcements

  • TAARIFA KWA UMMA February 19, 2025
  • TAARIFA KWA UMMA - MATUMIZI YA NISHATI SAFI YA KUPIKIA January 17, 2025
  • MATOKEO YA UPIMAJI WA KITAIFA WA DARASA LA NNE (SFNA) 2024 January 04, 2025
  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA KWANZA, 2025 December 16, 2024
  • View All

Latest News

  • Mwenge wa Uhuru waweka jiwe la Msingi Kituo cha Afya Mzinga

    June 03, 2025
  • Mwenge wa Uhuru wakagua mradi wa vijana "Ulipo Tupo" Tabata

    June 03, 2025
  • Mradi wa Ujenzi wa Barabara ya Magengeni - Chang'ombe umewekewa jiwe la msingi na Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru Kitaifa

    June 03, 2025
  • Mwenge wa Uhuru wazindua mradi wa Nishati Safi Soko la Samaki Feri

    June 03, 2025
  • View All

Video

Msimbazi Basin Development Project Implementation Area
More Videos

Quick Links

  • Former City Council Mayors
  • Motorcycle's Permit
  • Solid Waste Management
  • Smart Area
  • Dar es Salaam Centre for Architectural Heritage
  • Beaches, Waterfronts and Islands
  • Cultural Arts and Traditions
  • Historical and Heritage building and sites
  • Public spaces, Garden and Sports

Related Links

  • BUNGE
  • Blogu ya Jiji
  • UTUMISHI
  • State House
  • Ilala Municipal Council
  • Tanzania Information Services

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Location Map

Contact Us

    1 BARABARA YA MOROGORO 11882 DAR ES SALAAM

    Postal Address: S.L.P 20950

    Telephone: 0738 378 386

    Mobile: 0738 378 386

    Email: info@dcc.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclaimer
    • Sitemap

Copyright © 2017 Dar es Salaam City Council . All rights reserved.