• Contact Us |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
    • Complaints |
Dar es Salaam City Council
Dar es Salaam City Council

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government Dar es Salaam City Council

  • Home
  • About Us
    • City Profile
    • Mission and Vision
    • Core Values
    • Council Strategies
  • Administration
    • Organization Structure
    • Department
      • Finance, Administration and Personnel
      • Works and Fire Rescue
      • Waste Management
      • Urban Planning, Environment and Transportation
      • Health Services
    • Units
      • Planning, Monitoring and Statistics
      • Legal and Safety
      • Public Relations and Protocol
      • Internal Audit
      • Procurement and Supply
  • Investment Opportunity
    • Tourism Activities
      • Our Dar es Salaam
      • Animal zoos
      • Cultural Arts and Traditions
      • Dar es Salaam Centre for Architectural Heritage
      • Public spaces, Garden and Sports
      • Shopping, Entertainment and Social life
      • Historical and Heritage building and sites
      • Beaches, Waterfronts and Islands
    • Recycling of Solid Waste
  • Our Services
    • Motorcycle Permit
    • Taxi Parking Permit
    • Car Parking
    • Bus Terminals
    • Solid Waste Management
    • Land History Information
    • Burial for unclaimed dead bodies
  • Councillors
    • All Councillors
    • Standing Committee
      • Finance and Administration Committee
      • Urban Planning, Environment and Infrastructure Commitee
      • Planning and Coordination Committee
      • Social Welfare Committee
      • Ethics Committee
    • Council Meetings
    • Lord Mayor's Timetable
    • Former City Mayors
  • Projects
    • Completed projects
    • Planned Projects
    • Ongoing Projects
    • City Investments
  • Publications
    • Acts
    • ByLaws
    • Policies
    • Guidelines
    • Reports
    • Application Form
    • Integrity Pledges Form
  • Media Centre
    • Press Release
    • Photo Gallery
    • Video Gallery
    • Speeches
    • News
    • Events

Wilaya ya Ilala yafanya mdahalo kuadhimisha Miaka 61 ya Uhuru

Posted on: December 9th, 2022

Mkuu wa Wilaya ya Ilala Mhe. Ng'wilabuzu Ludigija leo tarehe 9 Disemba, 2022 ameshiriki kwenye mdahalo kujadili maendeleo mbalimbali yaliyopo katika Wilaya ya Ilala tangu kupatikana kwa Uhuru wa Nchi yetu hadi sasa.

Mdahalo huo umefanyika katika ukumbi wa Mikutano wa Karimjee ikiwa ni Siku ya Maadhimisho ya Miaka 61 ya Uhuru wa Tanzania Bara ambapo Mkuu wa Wilaya ya Ilala kwenye hotuba yake alisema "Katika miaka 61 ya Uhuru Ilala imefikia maendeleo makubwa sana ukiangalia Sekta ya Elimu hapo mwanzo Dar es Salaam kulikuwa na Shule Tano tu na zote zilikuwa Chini ya Wakoloni leo hii Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam katika Uongozi wa Dkt. Samia Suluhu Hassan kuna jumla ya Shule 106 ndani yake shule 60 ni za Serikali na shule 41 ni shule Binafsi, haya ni mafanikio makubwa sana katika Sekta ya Elimu"

Aidha, Mhe. Ludigija alitumia fursa hiyo kumshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia kwa kuipatia Wilaya ya Ilala fedha za ujenzi wa mabweni maalum "Namshukuru Rais Dkt Samia Suluhu Hassan katika kutoa pesa katika hizi ambazo kila miaka zinatumika katika sherehe za maadhimisho ya Uhuru na sasa zimeenda kujenga Mabweni ya shule Maalumu". Amesema Mhe. Ludigija.

Katika mdahalo huo mada mbalimbali zimewasilishwa kama vile kuhusu Elimu kutoka Uhuru hadi sasa, Siasa toka uhuru hadi sasa, uchumi na maendeleo kutoka Uhuru hadi sasa pamoja na kutathmini maendeleo katika miaka 61 ya uhuru wa Tanzania bara.

Akiwasilisha mada ya siasa na maendeleo Mstahiki Meya wa Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam amesema "Tuenzi maneno ya Mwalimu Julius Kambarage Nyerere lakini pia kupitia maadhimisho haya Mkuu wa Wilaya mpelekee salamu zetu Rais wetu Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kutoa Pesa Shilingi Bilioni 6.2 kwa ajili ya Ujenzi wa vyumba vya madarasa na naomba aendelee hivi hivi kwa miaka iliyobakia ili pesa ambazo zilikuwa zinafanya sherehe hizi kitaifa  ziende katika kuimarisha shughuli za maendeleo kwa kila Wilaya"

Katika kuimarisha siasa safi toka kipindi tunapata Uhuru tukiwa na chama kimoja hadi sasa Tanzania tuna jumla ya Vyama vya Siasa 22 vilivyosajiliwa kwa kudumu hii ni ishara yakuwa na siasa safi inayofanywa na Serikali ya Awamu ya Sita ikiwepo pia kuwatoa wanasiasa walioko magerezani kurudi uraiani na kufanya siasa.

Naye Mwenyekiti wa Baraza la Wazee Wilaya ya Ilala Mzee Matimbwa wakati akifanya wasilisho amesema "Kabla ya Uhuru hatukuwa na Chuo kikuu bali vyuo vilianza kupatikana kwa kuchangia kutoka kwa wananchi na kwa sasa tunaona namna Rais Dkt Samia Suluhu Hassan anatoa pesa kujenga madarasa kuendeleza elimu katika kuhimiza hilo kuwa misingi ya uongozi bora ni uaminifu na uzalendo wa kweli kwa kujali maslahi ya Nchi na ukiwa mzalendo na uzalendo ukiwepo hakutokuwa na rushwa kama tukiwa wazalendo tutaitekeleza siasa safi na nachukua nafasi hii kumpongeza Rais Dkt Samia Suluhu Hassan kwa kuenzi mambo yote kutoka wakati wa uhuru hadi leo kwa kusimamia kila zuri toka uhuru hadi sasa"

Mdahalo wa maadhimisho ya Miaka 61 ya Uhuru wa Tanzania Bara uliofanyika katika ukumbi wa Karimjee ulitanguliwa na matukio mbalimbali wakati wa juma la kilele cha Maadhimisho ya Sherehe za Miaka 61 ya Uhuru, matukio hayo ni pamoja na zoezi la upandaji miti katika Wilaya, mashindano ya Insha, usafi wa mazingira na shughuli za Kijamii, bonanza la michezo pamoja na mahojiano maalum na wazee huku maadhimisho hayo yakibeba kaulimbiu isemayo “Amani na Umoja ni Nguzo ya Maendeleo yetu”








Announcements

  • TAARIFA KWA UMMA February 19, 2025
  • TAARIFA KWA UMMA - MATUMIZI YA NISHATI SAFI YA KUPIKIA January 17, 2025
  • MATOKEO YA UPIMAJI WA KITAIFA WA DARASA LA NNE (SFNA) 2024 January 04, 2025
  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA KWANZA, 2025 December 16, 2024
  • View All

Latest News

  • "Tutahakikisha tunasimamia Kata 36 na Mitaa 159 ili Jiji la DSM liwe safi" - DC Mpogolo

    May 03, 2025
  • Jiji La DSM laweka mikakati kushinda UMITASHUMTA ngazi ya Mkoa

    April 29, 2025
  • Wakazi wa Jiji la Dar es Salaam waadhimisha Muungano kwa kupanda miti na kufanya usafi wa mazingira

    April 26, 2025
  • Zoezi la usafi wa mwisho wa wiki laendelea

    April 12, 2025
  • View All

Video

Msimbazi Basin Development Project Implementation Area
More Videos

Quick Links

  • Former City Council Mayors
  • Motorcycle's Permit
  • Solid Waste Management
  • Smart Area
  • Dar es Salaam Centre for Architectural Heritage
  • Beaches, Waterfronts and Islands
  • Cultural Arts and Traditions
  • Historical and Heritage building and sites
  • Public spaces, Garden and Sports

Related Links

  • BUNGE
  • Blogu ya Jiji
  • UTUMISHI
  • State House
  • Ilala Municipal Council
  • Tanzania Information Services

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Location Map

Contact Us

    1 BARABARA YA MOROGORO 11882 DAR ES SALAAM

    Postal Address: S.L.P 20950

    Telephone: 0738 378 386

    Mobile: 0738 378 386

    Email: info@dcc.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclaimer
    • Sitemap

Copyright © 2017 Dar es Salaam City Council . All rights reserved.