• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Dar es Salaam City Council
Dar es Salaam City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Mamlaka za Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya Jiji
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Fedha, Utawala na Utumishi
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Udhibiti Taka
      • Mipangomiji, Mazingira na Usafirishaji
      • Afya na Huduma za Tiba
    • Vitengo
      • Mipango, Ufuatiliaji na Takwimu
      • Sheria na Usalama
      • Itifaki, Uhusiano na Umma
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Ugavi na Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Shughuli za Utalii
      • Dar es Salaam Yetu
      • Misitu na Mashamba ya wanyama wafugwao
      • Sehemu za kitamaduni, ngoma za asili na sanaa za mikono
      • Kituo cha Urithi wa Ubunifu Majengo na Utalii
      • Maeneo ya kupumzika, bustani na viwanja vya michezo
      • Maeneo ya Manunuzi
      • Majengo na maeneo ya kihistoria
      • Uwanda wa bahari, fukwe na visiwa
    • Urejelezaji wa Taka Ngumu
  • Huduma Zetu
    • Vibali vya Pikipiki
    • Vibali vya Maegesho ya Teksi
    • Vibali vya Kuingiza Magari ya Mizigo
    • Vituo Vikuu vya Mabasi
    • Udhibiti Taka Ngumu
    • Taarifa za Historia ya Viwanja
    • Mazishi ya miili ya marehemu wasiokuwa na ndugu
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha na Uongozi
      • Kamati ya Mipangomiji, Mazingira na Miundombinu
      • Kamati ya Mipango na Ufuatiliaji
      • Kamati ya Huduma za Jamii
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba ya Vikao vya Kisheria
    • Ratiba ya Mstahiki Meya
    • Mameya Wazamani wa Jiji
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi iliyo kwenye Mpango
    • Miradi Inayoendelea
    • Vitega Uchumi vya Jiji
  • Machapisho
    • Sheria
    • Sheria Ndogo
    • Sera
    • Miongozo
    • Taarifa mbalimbali
    • Fomu za Maombi
    • Fomu za Ahadi ya Uadilifu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Hotuba
    • Habari Mpya
    • Matukio

DC Ilala azindua madarasa 310 yaliyojengwa kwa Fedha ya Pochi la Mama

Tarehe iliyowekwa: January 6th, 2023

Mkuu wa Wilaya ya Ilala Mhe. Ng'wilabuzu Ludigija, leo tarahe 06 Januari, 2023 amezindua Madarasa 10 yaliyokamilika katika Shule ya Sekondari Nguvu Mpya iliyopo Chanika Jijini Dar es Salaam, madarasa hayo ni miongoni mwa madarasa 310 yaliyojengwa kwa fedha ya Pochi la Mama, ambapo shule hiyo ilipokea kiasi cha Shilingi Milioni 200 kwa ajili ya ujenzi wa madarasa hayo 10, ofisi ya Walimu na ununuzi wa viti na meza.

Katika uzinduzi huo Mh. Ludigija amemshukuru Mheshimiwa  Rais Dkt. Samia Suluhu kwa kuipatia Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam kiasi cha Shilingi Bilion 6.2 kwa ajili ya ujenzi wa vyumba vya madarasa 310 "Namshukuru Mheshimiwa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kutuletea kiasi cha shilingi bil 6.2 kwa ajili ya ujenzi wa madarasa 310, kuanzia Jumatatu ambapo shule zinaenda kufunguliwa hakuna mtoto kwenye Halmashauri yetu ya Jiji la Dar es Salaam atakayeshindwa kuingia shuleni kwa sababu ya madarasa, Mama amefungua pochi na pochi lenyewe ndilo hili linaonekana” Amesema Mhe. Ludigija.

Naye Kaimu Mkurugenzi Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam, Mhandisi Amani Mafuru amesema Halmashauri imejipanga kwa kutenga kiasi cha Shilingi Milioni 700 kwa ajili ya kufidia idadi ya madawati yaliyopungua. Vilevile  itatumia mapato yake ya ndani  kwa kujenga  matundu ya vyoo kulingana na idadi ya ongezeko la wanafunzi kwa shule zilizopo Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam. Mhandisi Mafuru amemuhakikishia Mkuu wa Wilaya wa Ilala kuwa kila mtoto atakaa kwenye kiti na meza yake.

Naye Mbunge wa Jimbo la Ukonga, Mhe Jerry Silaa, ametoa pongezi nyingi kwa Mheshimiwa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwani fedha za Pochi la Mama zimesaidia wananchi hasa wanafunzi wa Jimbo lake kwa ujenzi madarasa ya shule zilizopo Jimbo la Ukonga, ambapo Jimbo hilo peke yake limepokea kiasi Shilingi billion 4.6. “Nitoe pongezi nyingi sana kwa Mheshimiwa Rais kwani Jimbo la Ukonga limependelewa tumepokea kiasi cha shilingi billion 4.6 na siyo kwamba limependelewa ni kwa sababu lina idadi kubwa ya watu.” Amesema Mhe. Silaa

Akihitimisha  Mkuu wa Shule ya Sekondari Nguvu Mpya, Bwana.Daniel Mwakyambiki amewataka walimu kuwa waadilifu na waaminifu wanapopokea fedha kwa ajili ya ujenzi kwa kufuata sheria na taratibu.

Matangazo

  • TAARIFA KWA UMMA February 19, 2025
  • TAARIFA KWA UMMA - MATUMIZI YA NISHATI SAFI YA KUPIKIA January 17, 2025
  • MATOKEO YA UPIMAJI WA KITAIFA WA DARASA LA NNE (SFNA) 2024 January 04, 2025
  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA KWANZA, 2025 December 16, 2024
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • "Tutahakikisha tunasimamia Kata 36 na Mitaa 159 ili Jiji la DSM liwe safi" - DC Mpogolo

    May 03, 2025
  • Jiji La DSM laweka mikakati kushinda UMITASHUMTA ngazi ya Mkoa

    April 29, 2025
  • Wakazi wa Jiji la Dar es Salaam waadhimisha Muungano kwa kupanda miti na kufanya usafi wa mazingira

    April 26, 2025
  • Zoezi la usafi wa mwisho wa wiki laendelea

    April 12, 2025
  • Angalia zote

Video

Msimbazi Basin Development Project Implementation Area
Video Zingine

Viunganishi vya Haraka

  • Mameya wa zamani wa Jiji
  • Vibali vya kuingia na Pikipiki katikati ya Jiji
  • Udhibiti wa Taka ngumu Jijini
  • Eneo Maalum la Usafi Jijini
  • Kituo cha Urithi wa Ubunifu Majengo na Utalii
  • Uwanda wa Bahari, Fukwe na Visiwa
  • Sehemu za Kitamaduni, Ngoma za Asili na Sanaa za Mikono
  • Majengo na Maeneo ya Kihistoria
  • Maeneo ya Kupumzika, Bustani na Viwanja vya Michezo

Viunganishi Linganifu

  • BUNGE
  • Blogu ya Jiji
  • UTUMISHI
  • IKULU
  • TAMISEMI
  • IDARA YA HABARI MAELEZO

Wasomaji mbalimbali duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    1 BARABARA YA MOROGORO 11882 DAR ES SALAAM

    Anuani ya Posta: S.L.P 20950

    Simu ya mezani: 0738 378 386

    Namba ya Mkononi: 0738 378 386

    Barua Pepe: info@dcc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki © 2017 Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam. Haki Zote Zimehifadhiwa.