Ofisi ya Mkurugenzi wa Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam leo, tarehe 21 Julai 2025, imepokea ugeni kutoka CAMFED Tanzania waliokuja kwa lengo la kujadili maendeleo ya wanafunzi wa kike wanaonufaika na mpango wa shirika hilo katika sekta ya elimu.
Wageni hao wamekutana na Mkurugenzi wa Jiji, Ndugu Elihuruma Mabelya, na kufanya mazungumzo mafupi kuhusu ushirikiano.
Mkurugenzi Mabelya amepongeza mchango wa CAMFED na kusisitiza umuhimu wa kuendeleza mashirikiano kati ya shirika hilo na Halmashauri ya Jiji, ili kuimarisha juhudi za serikali katika kuwawezesha watoto wa kike kielimu.
1 BARABARA YA MOROGORO 11882 DAR ES SALAAM
Anuani ya Posta: S.L.P 20950
Simu ya mezani: 0738 378 386
Namba ya Mkononi: 0738 378 386
Barua Pepe: info@dcc.go.tz
Hatimiliki © 2017 Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam. Haki Zote Zimehifadhiwa.