• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Dar es Salaam City Council
Dar es Salaam City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Mamlaka za Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya Jiji
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Fedha, Utawala na Utumishi
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Udhibiti Taka
      • Mipangomiji, Mazingira na Usafirishaji
      • Afya na Huduma za Tiba
    • Vitengo
      • Mipango, Ufuatiliaji na Takwimu
      • Sheria na Usalama
      • Itifaki, Uhusiano na Umma
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Ugavi na Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Shughuli za Utalii
      • Dar es Salaam Yetu
      • Misitu na Mashamba ya wanyama wafugwao
      • Sehemu za kitamaduni, ngoma za asili na sanaa za mikono
      • Kituo cha Urithi wa Ubunifu Majengo na Utalii
      • Maeneo ya kupumzika, bustani na viwanja vya michezo
      • Maeneo ya Manunuzi
      • Majengo na maeneo ya kihistoria
      • Uwanda wa bahari, fukwe na visiwa
    • Urejelezaji wa Taka Ngumu
  • Huduma Zetu
    • Vibali vya Pikipiki
    • Vibali vya Maegesho ya Teksi
    • Vibali vya Kuingiza Magari ya Mizigo
    • Vituo Vikuu vya Mabasi
    • Udhibiti Taka Ngumu
    • Taarifa za Historia ya Viwanja
    • Mazishi ya miili ya marehemu wasiokuwa na ndugu
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha na Uongozi
      • Kamati ya Mipangomiji, Mazingira na Miundombinu
      • Kamati ya Mipango na Ufuatiliaji
      • Kamati ya Huduma za Jamii
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba ya Vikao vya Kisheria
    • Ratiba ya Mstahiki Meya
    • Mameya Wazamani wa Jiji
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi iliyo kwenye Mpango
    • Miradi Inayoendelea
    • Vitega Uchumi vya Jiji
  • Machapisho
    • Sheria
    • Sheria Ndogo
    • Sera
    • Miongozo
    • Taarifa mbalimbali
    • Fomu za Maombi
    • Fomu za Ahadi ya Uadilifu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Hotuba
    • Habari Mpya
    • Matukio

Kamati ya fedha na utawala Jiji la DSM yafanya ziara ya ukaguzi wa miradi iliyotekelezwa kwa kipindi cha Januari-Machi, 2021

Tarehe iliyowekwa: May 4th, 2021

Na: Hashim Jumbe

Kamati ya Fedha na Utawala Halmashauri ya Jiji la DSM, leo tarehe 04 Mei, 2021 imefanya ziara ya ukaguzi wa Miradi ya Maendeleo iliyotekelezwa na Halmashauri hiyo kwa kipindi cha robo ya Tatu (3) ya kuanzia Januari hadi Machi, 2021, Kamati hiyo ambayo moja kati ya majukumu yake ni kuhakikisha Miradi yote ya Maendeleo inayotekelezwa kwenye Halmashauri inapata usimamizi wa kutosha ikiwa pamoja na kupima thamani halisi ya fedha zinazotumika kwenye Miradi hiyo.

Aidha, ziara hiyo ni ya kawaida na inatoa fursa kwa wajumbe wa Kamati hiyo kuweza kukagua na kutolea mapendekezo Miradi ya Maendeleo iliyotekelezwa na Halmashauri kwa kipindi husika.

"Leo tumefanya ziara na kamati ya fedha, lengo na madhumuni ni kukagua miradi yote ya kimkakati ambayo sisi tunaisimamia kama Jiji, na miradi hii ya kimkakati ni mwendelezo wa utekelezaji wa ilani ya Chama cha Mapinduzi ambayo iliahidi kwa Wananchi, tumeanzia kwenye machinjio ya vingunguti ambapo kule mradi umegharimu takribani Bilioni 12.48 na hatua iliyobaki ni kuweka zege nje" alisema Mhe. Omary Kumbilamoto, Mstahiki Meya wa Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam

Lakini pia kamati ya fedha na utawala ilitembelea na mradi wa pili wa kimkakati ambao ni Ujenzi wa Soko la Kisutu, ambapo Mstahiki Meya Kumbilamoto alieleza "tumekuja kutembelea ujenzi wa mradi wa Soko la Kisutu, mradi huu una thamani ya takribani Bilioni 13.49 na teyari mradi umefikia 97% kinachosubiriwa hapa ni 'lift' na tunatumaini wafanyabiashara mwishoni mwa mwezi huu wanaweza kuingia"

Mhe. Kumbilamoto aliendelea kueleza kuwa "mwanzo tuliwakuta wafanyabiashara 669, lakini niwashukuru Serikali Kuu na Waheshimiwa Madiwani, hivi sasa Soko hili litabeba wafanyabiashara zaidi ya 1,500 maana yake tutaongeza mapato makubwa sana kwa Jiji letu la DSM na kutatua kero nyengine ambazo wananchi zinawakabili"

Itakumbukwa kuwa Kamati ya Fedha na Utawala ina jukumu la kusimamia miradi yote ya Halmashauri katika sekta ya elimu, afya, maji, kilimo, ufugaji pamoja na kuhakikisha 10% ya mikopo kwa wanawake, vijana na watu wenye ulemavu inatolewa na Halmashauri kwa walengwa

Ziara hiyo itafuatiwa na kikao cha kamati kitakachojadili taarifa za utendaji kazi kwa idara na vitengo wanavyovisimamia pamoja na kupitia na kujadili taarifa ya miradi iliyotekelezwa kwa kipindi cha Januari hadi Machi, 2021

Matangazo

  • TAARIFA KWA UMMA February 19, 2025
  • TAARIFA KWA UMMA - MATUMIZI YA NISHATI SAFI YA KUPIKIA January 17, 2025
  • MATOKEO YA UPIMAJI WA KITAIFA WA DARASA LA NNE (SFNA) 2024 January 04, 2025
  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA KWANZA, 2025 December 16, 2024
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • "Tutahakikisha tunasimamia Kata 36 na Mitaa 159 ili Jiji la DSM liwe safi" - DC Mpogolo

    May 03, 2025
  • Jiji La DSM laweka mikakati kushinda UMITASHUMTA ngazi ya Mkoa

    April 29, 2025
  • Wakazi wa Jiji la Dar es Salaam waadhimisha Muungano kwa kupanda miti na kufanya usafi wa mazingira

    April 26, 2025
  • Zoezi la usafi wa mwisho wa wiki laendelea

    April 12, 2025
  • Angalia zote

Video

Msimbazi Basin Development Project Implementation Area
Video Zingine

Viunganishi vya Haraka

  • Mameya wa zamani wa Jiji
  • Vibali vya kuingia na Pikipiki katikati ya Jiji
  • Udhibiti wa Taka ngumu Jijini
  • Eneo Maalum la Usafi Jijini
  • Kituo cha Urithi wa Ubunifu Majengo na Utalii
  • Uwanda wa Bahari, Fukwe na Visiwa
  • Sehemu za Kitamaduni, Ngoma za Asili na Sanaa za Mikono
  • Majengo na Maeneo ya Kihistoria
  • Maeneo ya Kupumzika, Bustani na Viwanja vya Michezo

Viunganishi Linganifu

  • BUNGE
  • Blogu ya Jiji
  • UTUMISHI
  • IKULU
  • TAMISEMI
  • IDARA YA HABARI MAELEZO

Wasomaji mbalimbali duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    1 BARABARA YA MOROGORO 11882 DAR ES SALAAM

    Anuani ya Posta: S.L.P 20950

    Simu ya mezani: 0738 378 386

    Namba ya Mkononi: 0738 378 386

    Barua Pepe: info@dcc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki © 2017 Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam. Haki Zote Zimehifadhiwa.