• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Dar es Salaam City Council
Dar es Salaam City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Mamlaka za Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya Jiji
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Fedha, Utawala na Utumishi
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Udhibiti Taka
      • Mipangomiji, Mazingira na Usafirishaji
      • Afya na Huduma za Tiba
    • Vitengo
      • Mipango, Ufuatiliaji na Takwimu
      • Sheria na Usalama
      • Itifaki, Uhusiano na Umma
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Ugavi na Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Shughuli za Utalii
      • Dar es Salaam Yetu
      • Misitu na Mashamba ya wanyama wafugwao
      • Sehemu za kitamaduni, ngoma za asili na sanaa za mikono
      • Kituo cha Urithi wa Ubunifu Majengo na Utalii
      • Maeneo ya kupumzika, bustani na viwanja vya michezo
      • Maeneo ya Manunuzi
      • Majengo na maeneo ya kihistoria
      • Uwanda wa bahari, fukwe na visiwa
    • Urejelezaji wa Taka Ngumu
  • Huduma Zetu
    • Vibali vya Pikipiki
    • Vibali vya Maegesho ya Teksi
    • Vibali vya Kuingiza Magari ya Mizigo
    • Vituo Vikuu vya Mabasi
    • Udhibiti Taka Ngumu
    • Taarifa za Historia ya Viwanja
    • Mazishi ya miili ya marehemu wasiokuwa na ndugu
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha na Uongozi
      • Kamati ya Mipangomiji, Mazingira na Miundombinu
      • Kamati ya Mipango na Ufuatiliaji
      • Kamati ya Huduma za Jamii
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba ya Vikao vya Kisheria
    • Ratiba ya Mstahiki Meya
    • Mameya Wazamani wa Jiji
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi iliyo kwenye Mpango
    • Miradi Inayoendelea
    • Vitega Uchumi vya Jiji
  • Machapisho
    • Sheria
    • Sheria Ndogo
    • Sera
    • Miongozo
    • Taarifa mbalimbali
    • Fomu za Maombi
    • Fomu za Ahadi ya Uadilifu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Hotuba
    • Habari Mpya
    • Matukio

RC Makalla aagiza wasimamizi, mkandarasi kukamilisha ujenzi wa machinjio ya kisasa Vingunguti kwa wakati

Tarehe iliyowekwa: June 9th, 2022

Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Mh. Amos Makalla, amewaagiza wasimamizi na mkandarasi katika machinjio ya kisasa ya Vingunguti kusimamia kwa umakini ukamilishaji wa machinjio hiyo. Mheshimiwa Makalla ameagiza hivyo alipofanya ziara katika machinjio hiyo leo Juni 9, 2022.

“Namshukuru Rais wetu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mh. Samia Suluhu Hassan kwa fedha nyingi alizozitoa katika ujenzi wa machinjio ya Vingunguti. Hivyo naomba ujenzi wa machinjio hayo ukamilike kwa muda uliopangwa. Ni matarajio yangu kwamba kwamba mkandrasi atafanya kazi usiku na mchana kukamilisha ujenzi ili tuanze kufanya biashara ya kuuza nyama kimataifa”.

Mkuu huyo wa Mkoa, alikagua kazi iliyokwisha fanya na kuelekeza kwamba vyumba vya kuhifadhia nyama kwa ajili ya biashara kimataifa, ujenzi wa tanki la maji, maeneo ya kuwekea mbolea vikamilishwe haraka. Aidha, aliwataka wafanyabiashara ya nyama katika machinjio hiyo kutambua hadhi ya machinjio ya vingunguti ambayo itakidhi malengo ya biashara kutokana na uwezo mkubwa wa machinjio. Katika machinjio hiyo ng’ombe wapatao elfu moja na mbuzi mia tano wanaweza kujichwa kwa wakati mmoja.

Aliwataka wafanya biashara hao kubadilika na kuzitumia vema fursa zinazotokana na machinjio hiyo. “Wafanyabiashara mbadilike, mfanye biashara kuendana na machinjio hii ya kisasa ikiwa na mazingira mazuri ya utendaji kazi. Acheni kufanya kazi kwa mazoea tunatakiwa kubadilika na kufanya kazi katika mabucha hayo ya kisasa,” alisema Mheshimiwa Makalla.

Kupitia ziara hiyo, Mkuu wa Wilaya ya Ilala, Mh. Ng’wilabuzu Ludigija, alimshukuru Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam kwa kufanya ziara hiyo. “Nashukuru ujio wako Mheshimiwa Mkuu wa Mkoa katika machinjio yetu ya Vingunguti. Umefanya ziara katika machinjio hii mara kwa mara kuona nini kinaendelea na kwa kiasi kikubwa tumepambana kuhakikisha mabucha ya sehemu ya machinjio hii yanakamilika kwa mujibu wa makubaliano tuliyofikikia ili wafanyabiashara waweze kuhamia katika machinjio hii mpya,” alisema Mheshimiwa Ludigija.

Matangazo

  • TAARIFA KWA UMMA February 19, 2025
  • TAARIFA KWA UMMA - MATUMIZI YA NISHATI SAFI YA KUPIKIA January 17, 2025
  • MATOKEO YA UPIMAJI WA KITAIFA WA DARASA LA NNE (SFNA) 2024 January 04, 2025
  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA KWANZA, 2025 December 16, 2024
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • "Tutahakikisha tunasimamia Kata 36 na Mitaa 159 ili Jiji la DSM liwe safi" - DC Mpogolo

    May 03, 2025
  • Jiji La DSM laweka mikakati kushinda UMITASHUMTA ngazi ya Mkoa

    April 29, 2025
  • Wakazi wa Jiji la Dar es Salaam waadhimisha Muungano kwa kupanda miti na kufanya usafi wa mazingira

    April 26, 2025
  • Zoezi la usafi wa mwisho wa wiki laendelea

    April 12, 2025
  • Angalia zote

Video

Msimbazi Basin Development Project Implementation Area
Video Zingine

Viunganishi vya Haraka

  • Mameya wa zamani wa Jiji
  • Vibali vya kuingia na Pikipiki katikati ya Jiji
  • Udhibiti wa Taka ngumu Jijini
  • Eneo Maalum la Usafi Jijini
  • Kituo cha Urithi wa Ubunifu Majengo na Utalii
  • Uwanda wa Bahari, Fukwe na Visiwa
  • Sehemu za Kitamaduni, Ngoma za Asili na Sanaa za Mikono
  • Majengo na Maeneo ya Kihistoria
  • Maeneo ya Kupumzika, Bustani na Viwanja vya Michezo

Viunganishi Linganifu

  • BUNGE
  • Blogu ya Jiji
  • UTUMISHI
  • IKULU
  • TAMISEMI
  • IDARA YA HABARI MAELEZO

Wasomaji mbalimbali duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    1 BARABARA YA MOROGORO 11882 DAR ES SALAAM

    Anuani ya Posta: S.L.P 20950

    Simu ya mezani: 0738 378 386

    Namba ya Mkononi: 0738 378 386

    Barua Pepe: info@dcc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki © 2017 Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam. Haki Zote Zimehifadhiwa.